Google AdSense

Breaking News

Penalt za kifundi kabisa Singida united vs Green warriors FA Cup


Baada ya kushindwa kufungana kwa  timu zote mbili japo Singida united walionekana wakishambulia sana lango la maafande hao wa mbweni ila pengine upungufu wao ulisababisha kutokupata goli baada ya mshambuliaji wao aliyeonesha kiwango kizuri mapema tu mwa mchezo Kambale Selita kuoneshwa kadi nyekundu dakika ya 23 baada ya kumrushia ngumi beki wa Green warriors wakati wakisukumana mpira wa kona
Dakika 90 zilimalizika na kwenda kupiga mikwaju ya penalt ambapo Singida united walionekana wakiwa na uhakika zaidi kwenye upigaji penalt Green warriors walikosa penalt mbili moja golikipa Ali Mustapha  (Batez) akipangua huku nyingine wakigongesha mwamba wa pembeni na mpira kutoka nje na kufanya matokeo kuwa (3-4) 
Nakuwafanya matajiri hao wa singida timu inayotoa burudani ikiwa kiwanjani chini ya kocha Hance pluijin kupanda hatua inayofuata ikumbukwe hawa Green warriors ndio waliowatoa mabingwa watetezi wa kombe hilo Simba SC.  

No comments